Saturday, August 8, 2009

Kuwaona Villa Elfu Hamsini

Timu ya simba sports club leo imetangaza kiingilio cha kwenye tamasha la timu hiyo itakapopambana na timu ya sport villa ya uganga katika mchezo utakaofanyika jumapili wiki hii katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa wekundu hao hasan Dalali amesema kuwa kiingilio cha juu kitakuwa shilingi elfu 50 wakatiki kile cha chini kitakuwa shilingi eltu 3

Dalali amesema kuwa siku ya pambano hilo ambalo litakuwa na lengo la kuitambulisha timu ya simba sambamba na kuwatambulisha wachezaji wapya, ambapo mgeni rasimi atakuwa spika wa bungu la jamhuri ya muungano wa Tanzania samwel sitta

Sambamba na hilo club ya simba imelitaka shirikisho la soka nchini tff kuwaruhusu wachezaji waliochaguliwa kucheza timu ya taifa stars kujiunga na timu hiyo augast 9 badala ya siku ya leo kama ilivyokuwa imetangazwa.

Simba waigomea stars
Katibu mkuu wa simba mwina kaduguda amesema kuwa sababu ya kufanya hivyo ni kuwaandaa wachezaji wa klab hiyo katika maaandalizi ya ligi kuu Tanzania bara inayotaarajiwa kuanza kutimua vumbi augast 23 mwaka huu wakiwa chini ya kocha wao.

Wachezaji saba wa timu ya simba walioitwa katika timu ya tafifa ya Tanzania taifa stars ni ally Mustapha, kelvini yondan, david naftari, juma jabu, juma nyoso, musa hasan mgosi na danny mrwanda.


soka
Timu ya davis conner leo imetoa kichapo kwa timu ya mchanagani kwa kuifunga jumla ya boa 2-1 katika mchezo wa ligi ya kombe la upendo uliofanyika katika uwanja wa tandika mabatini jijini Dar es salaam.

Mabao ya davis conner yalifungwa na mashaka mahira katika dk ya 11 na 26 wakati lile la kuondoa aibu la mchangani lilipachikwa wavuni na abuu azizi katika dakika 52.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho wakati watani wa jadi wa ligi hiyo wataingia uwanjani kuonyeshana ubabe wa nani mkali kati ya timu ya taitanic sports club na home boys team katika mchezo utakaopigwa pale pale katika uwanja wa tandika mabatini.

Nayo mashindano la kombe la maembe (maembe cup) imeendelea leo hatua ya robo fainali ambapo timu ya ya hali ya hewa imewachapa kitintale bao 1-0 katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi yombo kiwalani.

No comments:

Post a Comment